Uteuzi wa Kidato cha Kwanza uwe wa haki

WALIMU Wakuu wa shule za upili, hasa za ngazi ya taifa, wanakutana leo (Ijumaa), kuanza kuwateua wanafunzi
watakaojiunga na kidato cha kwanza.
Uteuzi huo umeibua hisia kali, hasa kutoka kwa wadau katika sekta ya shule za kibinafsi.
Mwenyekiti wa chama cha Shule za Kibinafsi Bw John Mwai, ametishia kwenda mahakamani iwapo Serikali itaendelea na
mpango wa kuteua mwanafunzi mmoja kutoka shule za kibinafsi kwa kila watatu kutoka za umma.
Huenda shule za kibinafsi zikawa na hoja katika jambo hili. Watoto waliosoma katika shule za kibinafsi, bado ni
watoto wa Kenya. Kama walipata alama za kuwawezesha kujiunga na shule za kitaifa, hakuna sababu ya kuwanyima.
Lakini pia Bw Mwai na wenzake wanafaa kujiuliza; ikiwa mwanafunzi aliyesoma akiwa anakalia mawe atapata alama 380
na aliyekuwa akibebwa kwa gari, akisoma kwenye shule yenye vifaa vyote atapata alama 390, ni yupi anayestahili
nafasi katika shule ya kitaifa?
Katiba yetu inasema elimu ni haki ya kila mtoto bila kubaguliwa. Kwa hivyo, mtoto wa maskini aliyesoma katika shule
ya umma, akinyimwa nafasi hiyo, hawezi kwenda kupata nafasi katika shule nzuri ya upili ya kibinafsi.
Nayo Serikali kwa upande wake, inapaswa kuhakikisha kuwa inakamilisha pesa ilizoahidi kuzipa shule zilizopandishwa
ngazi majuzi.
Hakutakuwa na usawa kama mwanafunzi mmoja aliyepata alama 400 ataitwa kujiunga na Alliance au Mangu na mwenzake
aliyepata alama sawa na hizo ajiunge na Pangani, Maranda au Shimo La Tewa, ikiwa shule hizi hazitapewa vifaa vinavyohitajika kufaulisha masomo.Bila shaka, mwanafunzi aliye shule za kitaifa za kundi la kwanza atakuwa amemzidi mwenzake.
Shule za ngazi ya mkoa na wilaya pia zinafaa kufadhiliwa na Serikali ili viwango vya elimu viimarike katika shule
za umma.

 

Audio Pdf video

Kina mama jitokezeni

Akina mama wanastahili kujitokeza kuwania nyadhifa mbalimbali wakati wa uchaguzi mkuu ujao.
Kauli hiyo ilitolewa na diwani wa wadi ya Shanzu, kaunti ya Mombasa, Bi Maimuna Salim, hapo jana.
Alisema kwamba akina mama ndio uti wa mgongo wa taifa hili, na wanapswa kujitokeza kukabiliana ana kwa ana na wanaume bila kusubiri kuteuliwa.
Sawa na wanaume, akina mama pia wana uwezo,juhudi na maarifa ya kuleta mendeleo nchini, alinena Bi Maimuna.
Alitoa mwito kwa vijana wajihadhari ili wasiumiwe na wanasiasa kuzua fujo wakati huu ambapo uchaguzi mkuu unakaribia.
Bi Maimuna alikuwa akizungumza katika hafla fupi ya uzinduzi wa mataa ya barabarani katika wadi hiyo, iliyofanyika katika eneo la Saga karibu na hoteli ya kitalii ya Severin.
Wakati huo huo, Bi Maimuna aliwaonya vikali mabwanyenye wanaoziba njia za wananchi kutumia kuelekea ufuoni kwamba siku zao zimefika.
Alisema kwamba ingawa serikali ilitenga nafasi ya njia kwa wananchi kupitia kuelekea ufuoni kujivinjari na wavuvi kuelekea baharini, sasa nafasi hizo zimenyakuliwa na mabwanyenye.
Alishangaa kwamba barabara hizo ndogo zimezibwa na mabwanyenye hao hivyo kuwalazimisha wananchi kutembea mbali ili kufika ufuoni.
Aidha, diwani huyo aliwataka wananchi kuwa na subira wakati huu anaposhghulikia swala hilo, huku akiahidi kwamba suluhisho litapatikana hivi karibuni.

 

Audio

 

Student Expirience

ICC: Kamati itekeleze haki

 

WAKENYA wanaposubiri uamuzi wa Mahakama ya Kimataifa ya ICC kuhusu washukiwa

 

 

Student Expirience

Man and Woman jumping off a cliff into a river

Uteuzi wa Kidato cha Kwanza uwe wa haki

 

WALIMU Wakuu wa shule za upili, hasa za ngazi ya taifa, wanakutana leo

 

 

http://syndication.nation.co.ke