Rais wa Ujerumani ajiuzulu kuhusiana na ufisadi

Rais wa Ujerumani Christian Wulff

Picha/AFP Rais wa Ujerumani Christian Wulff (Kushoto) akiongea kando mwa mkewe Bettina alipotangaza kuwa amejiuzulu Ijumaa. 

Na XINHUA  ( email Mwandishi)

Imepakiwa - Friday, February 17  2012  at 19:51

Kwa Mukhtasari

Christian Wulff alijiuzulu baada ya viongozi wa mashtaka kuliomba bunge la Ujerumani limwondolee kinga dhidi ya mashtaka, jambo ambalo lingepelekea yeye kuchunguzwa rasmi kuhusiana na madai ya ufisadi. Anadaiwa kuchukua mkopo kutoka mke wa rafiki yake kwa riba ya chini 2008.

 

BERLIN, Ujerumani

CHANSELA wa Ujerumani, Angela Merkel, Ijumaa alieleza masikitiko makubwa kufuatia kujiuzulu kwa Rais Christian Wulff.

Kiongozi huyo alijiuzulu kufuatia mzozo ulitokana na mkopo wa kibinafsi ambao alikuwa ameuchukua.

Nusu saa tu, baada ya Wulff kutangaza kujiuzulu kwake, Merkel, kwenye taarifa alimshukuru rais huyo kutokana na mchango wake na kusema anaheshimu uamuzi wake.

Alisema atashauriana na Serikali, vyama vya kisiasa kutafuta atayechukua wadhifa wa Wulff.

Mashtaka

Wulff, 52, alitangaza kujiuzulu kwake kwenye kwenye televisheni, baada ya viongozi wa mashtaka kuliomba bunge la Ujerumani limwondolee kinga dhidi ya mashtaka, jambo ambalo lingepelekea yeye kuchunguzwa rasmi kuhusiana na madai ya ufisadi.

Wulff, alikuwa mshirika wa karibu wa Merkel, lakini alikabiliwa na shinikizo ilipobainika kuwa alijaribu kuzima ufichuzi wa gazeti la Bild, kuhusu mkopo aliouchukua 2008 kutoka kwa mke wa rafiki yake kwa riba ya chini mno.

Share Bookmark Print

Rating

 

 

 

 

 

 

Most Popular

Wabunge 175 kutahiriwa Zimbabwe

Wabunge 175 nchini Zimbabwe watapashwa tohara kufikia mwisho wa mwezi ujao katika juhudi za kuhamasisha wanaume

Mwanawe Waziri wa Fedha ajitia kitanzi

MWANAWE Waziri wa Fedha Njeru Githae anadaiwa kujiua nyumbani kwao Runda, Nairobi. Polisi wameanzisha uchunguzi

Polisi waendelea kusaka walioshambulia Mombasa

Polisi wameanzisha msako mkali kutafuta washukiwa waliotekeleza shambulio la kigaidi katika mkahawa wa Bella Vista,

Utengano wakumba ukumbusho wa Wanjiru

Ibada mbili tofauti zilifanywa kuadhimisha mwaka mmoja tangu kifo cha bingwa wa marathon katika Olimpiki Samuel