HABARI ZA SIASA
Na Na JOHN KIMWERE ( email Mwandishi)
Imepakiwa - Thursday, February 2 2012 at 23:17Kwa Mukhtasari
Wabunge hao wametishia kuungana na wenyeji wa mtaa wa Mukuru kwa Njenga, kufanya maandamano hadi katika afisi ya Waziri wa Usalama wa Ndani, Bw George Saitoti.
WABUNGE watano wakiongozwa na mawaziri wasaidizi, Bw Ferdinard Waititu na Bi Wavinya Ndeti, wamempatia kamshina wa Polisi, Bw Mathew Iteere, hadi kesho kutia nguvuni polisi waliohusika na mauaji Mukuru.
Wabunge hao wametishia kuungana na wenyeji wa mtaa wa Mukuru kwa Njenga, kufanya maandamano hadi katika afisi ya Waziri wa Usalama wa Ndani, Bw George Saitoti, iwapo Iteere atashindwa kuwakamata waliohusika na mauaji hayo.
Wiki jana, wakazi watatu wa mtaa huu walipigwa risasi katika ubomoaji ambao ambao ulisitishwa punda baada ya kuanza.
Wabunge hao walisema hayo, kwenye mkutano uliofanyika katika uwanja wa eneo kulikofanyika ubomoaji huo Jumatano jioni.
Bw Waititu aidha, alikuwa ameandamana na Wabunge Gideon Mbuvi, John Mututho na Yusuf Hassan.
“Tutashirikiana na wenzangu Bw Waititu na Bi Ndeti kugharamia mazishi ya waliokufa kwenye ghasia hizo,” alisema Bw Sonko.
Aliongezea kwamba watahakikisha vijana wote waliokamatwa wakati huo wameachiliwa.
Aidha wabunge hao waliwakikishia wenyeji kwamba hakuna ubomoaji utafanyika eneo hilo.
Wabunge 175 nchini Zimbabwe watapashwa tohara kufikia mwisho wa mwezi ujao katika juhudi za kuhamasisha wanaume
MWANAWE Waziri wa Fedha Njeru Githae anadaiwa kujiua nyumbani kwao Runda, Nairobi. Polisi wameanzisha uchunguzi
Polisi wameanzisha msako mkali kutafuta washukiwa waliotekeleza shambulio la kigaidi katika mkahawa wa Bella Vista,
Ibada mbili tofauti zilifanywa kuadhimisha mwaka mmoja tangu kifo cha bingwa wa marathon katika Olimpiki Samuel