HABARI ZA SIASA
Na LUCAS BARASA ( email Mwandishi)
Imepakiwa - Friday, February 3 2012 at 22:33Kwa Mukhtasari
Waziri wa Mashauri ya Nchi za Kigeni wa Uingereza, Bw William Hague, amefurahishwa kwa kurejea kwa utulivu Mogadishu na sehemu nyingine za nchi hiyo.
UINGEREZA imeitaka jamii ya kimataifa itumie fursa ya usalama Somalia kuimarisha uthabiti nchini humo.
Waziri wa Mashauri ya Nchi za Kigeni wa Uingereza, Bw William Hague, aliyefika nchini jana alisema nchi yake imefurahishwa kwa kurejea kwa utulivu Mogadishu na sehemu nyingine za nchi hiyo.
Hii imetokana na juhudi za walinda usalama wa Muungano wa Afrika (Amisom), wale wa Serikali ya Mpito ya Somalia (TFG) na Majeshi ya Ulinzi ya Kenya (KDF) dhidi ya wanamgambo wa kundi la Al-Shabaab.
“Usalama umeimarika. Nilijionea mwenyewe jana (Alhamisi),” akasema. Alikuwa mjini Mogadishu kabla ya kutua Kenya kukutana na Rais Mwai Kibaki.
Alisema raia wa Somalia wanatamani amani baada ya miaka mingi ya mapigano. Alisema Uingereza itatetea kuunganishwa kwa majeshi ya Kenya na yale ya Amisom katika mkutano wa baraza la Umoja wa Mataifa.
Wabunge 175 nchini Zimbabwe watapashwa tohara kufikia mwisho wa mwezi ujao katika juhudi za kuhamasisha wanaume
MWANAWE Waziri wa Fedha Njeru Githae anadaiwa kujiua nyumbani kwao Runda, Nairobi. Polisi wameanzisha uchunguzi
Polisi wameanzisha msako mkali kutafuta washukiwa waliotekeleza shambulio la kigaidi katika mkahawa wa Bella Vista,
Ibada mbili tofauti zilifanywa kuadhimisha mwaka mmoja tangu kifo cha bingwa wa marathon katika Olimpiki Samuel