HABARI ZA SIASA
Na JOYCE BOKE ( email Mwandishi)
Imepakiwa - Friday, February 10 2012 at 19:27Kwa Mukhtasari
Mamia ya wazazi wanamiminika maduka ya sare mjini Nakuru huku msimu wa kujiunga na kidato cha kwanza kwa wanafunzi waliofanya Mtihani wa Kitaifa wa Darasa la Nane (KCPE) mwaka jana ukiwa umeshika kasi.
HUKU msimu wa kujiunga na kidato cha kwanza kwa wanafunzi waliofanya Mtihani wa Kitaifa wa Darasa la Nane (KCPE) mwaka jana ukiwa umeshika kasi, mamia ya wazazi walimiminika maduka ya sare mjini Nakuru.
Foleni ndefu zilishuhudiwa madukani humo hadi nje na barabani huku baadhi ya wazazi na wanao wakikosa kupata sare hizo kutokana na uhaba. Katika duka la Shah Outfitters na lile la Nakuru Wool shopping ni wanafunzi tu walioruhusiwa kuingia ndani ilihali wazazi walilazimika kuongoja nje ili kuzuia msongamano.
Wazazi walilalamika kuwa walilazimika kupanga foleni kwa hadi masaa manne na walipofika ndani wakajulishwa kuwa sare za mashule yao hazikuwepo au kuwa zilikuwa zimenunuliwa zikaisha. Walinzi walikuwa na wakati mgumu kumudu idadi hiyo na kuwatuliza wazazi waliokuwa na hasira baada ya kukosa sare za wanao.
Msimamizi wa mauzo katika duka la Nakuru Wool Shopping Martin Jaoko alisema kuwa uhaba huo umetokana na mashule kubadilisha sare zao bila kuwajulisha wauzaji na kucheleweshwa kwa sare hizo kutoka kwa makampuni ya utengenezaji.
Wabunge 175 nchini Zimbabwe watapashwa tohara kufikia mwisho wa mwezi ujao katika juhudi za kuhamasisha wanaume
MWANAWE Waziri wa Fedha Njeru Githae anadaiwa kujiua nyumbani kwao Runda, Nairobi. Polisi wameanzisha uchunguzi
Polisi wameanzisha msako mkali kutafuta washukiwa waliotekeleza shambulio la kigaidi katika mkahawa wa Bella Vista,
Ibada mbili tofauti zilifanywa kuadhimisha mwaka mmoja tangu kifo cha bingwa wa marathon katika Olimpiki Samuel