HABARI ZA SIASA

Serikali yapiga jeki shirika la reli

Na PETER MWAI  ( email Mwandishi)

Imepakiwa - Friday, February 10  2012  at 19:31

Kwa Mukhtasari

SERIKALI imebadilisha deni ambalo inadai Shirika la Reli la Kenya (KRC) kuwa mchango wake wa kifedha (mtaji) na kuimarisha udhibiti wake katika shirika hilo.

SERIKALI imebadilisha deni ambalo inadai Shirika la Reli la Kenya (KRC) kuwa mchango wake wa kifedha (mtaji) na kuimarisha udhibiti wake katika shirika hilo.

Hatua hiyo inatarajiwa kuimarisha shughuli za shirika hilo ambalo linategemewa kutekeleza jukumu muhimu Kenya inapojiandaa kutimiza Ruwaza ya 2030. Baraza la Mawaziri liliidhinisha hatua hiyo Alhamisi kwenye mkutano ulioandaliwa chini ya uongozi wa Rais Mwai Kibaki katika Ikulu ya Nairobi.

“Mawaziri wameidhinisha kubadilishwa kwa hesabu ya kifedha ya Shirika la Reli la Kenya. Hii itahusisha kubadilishwa kwa deni ambalo Serikali inalidai shirika hilo kuwa mtaji. Hatua hii itaondolea shirika hilo mzigo na kuliwezesha kuwa na msingi thabiti,” ilisema taarifa ya Chumba cha Habari cha Rais (PPS).

Mkopo

Kufikia Novemba 2005, serikali ilikuwa imelikopesha shirika hilo Sh14 bilioni. Kwa jumla, shirika lilikuwa likidaiwa Sh20 bilioni na wadeni mbalimbali.

Shirika hilo humiliki na kusimamia miundo msingi ya reli ambayo hukodisha kwa wahudumu wa reli.

Nchini, mfano ni kampuni ya Rift Valley Railways (RVR) ambayo ilikabidhiwa kandarasi ya kusimamia uchukuzi wa reli Kenya na Uganda kwa muda wa miaka 25 kuanzia 200.

Kuiamrisha huduma

Ujenzi wa reli ya kutumiwa kuimarisha huduma Nairobi unapangiwa kugharimu Sh16 bilioni, huku ule wa kujengwa reli ya kisasa kote nchini ukipangiwa kugharimu Sh320 bilioni.

Uchukuzi wa gari moshi una mchango mkubwa na muhimu katika kufanikisha uchukuzi wa mizigo na bidhaa nchini.

Katika jiji la Nairobi, unapangiwa kupunguza msongamano na pia uharibifu unaotokana na kupitishiwa kwa mizigo mizito kwenye barabara za lami.

Kadhalika, serikali imekuwa na mipango ya kubadilisha kabisa mfumo wa reli nchini kufikia mwaka wa 2050.

 

Most Popular

Wabunge 175 kutahiriwa Zimbabwe

Wabunge 175 nchini Zimbabwe watapashwa tohara kufikia mwisho wa mwezi ujao katika juhudi za kuhamasisha wanaume

Mwanawe Waziri wa Fedha ajitia kitanzi

MWANAWE Waziri wa Fedha Njeru Githae anadaiwa kujiua nyumbani kwao Runda, Nairobi. Polisi wameanzisha uchunguzi

Polisi waendelea kusaka walioshambulia Mombasa

Polisi wameanzisha msako mkali kutafuta washukiwa waliotekeleza shambulio la kigaidi katika mkahawa wa Bella Vista,

Utengano wakumba ukumbusho wa Wanjiru

Ibada mbili tofauti zilifanywa kuadhimisha mwaka mmoja tangu kifo cha bingwa wa marathon katika Olimpiki Samuel