Wawili kizimbani kwa madai ya kuroga

Na JAMES KARIUKI  ( email Mwandishi)

Imepakiwa - Thursday, February 16  2012  at 19:14

Kwa Mukhtasari

WATU wawili wanaodaiwa walisafiri kutoka Kisii hadi Kaunti ya Laikipia ili kuwaroga jamaa waliokosa kulipa deni, Alhamisi walishtakiwa kwa uchawi katika mahakama ya Nyahururu.

 

WATU wawili wanaodaiwa walisafiri kutoka Kisii hadi Kaunti ya 

WATU wawili wanaodaiwa walisafiri kutoka Kisii hadi Kaunti ya Laikipia ili kuwaroga jamaa waliokosa kulipa deni, Alhamisi walishtakiwa kwa uchawi katika mahakama ya Nyahururu.

Laikipia ili kuwaroga jamaa waliokosa kulipa deni, Alhamisi walishtakiwa kwa uchawi katika mahakama ya Nyahururu.

Lakini wawili hao, Bi Judith Nasu Watila, 49  na “mwelekezi wake” Bw Justus Nyakora Mwebi, 40 walikanusha mashtaka hayo mbele ya hakimu mkaazi, Bw Vincent Kiptoon.

Wawili hao waliwachiliwa kwa dhamana ya Sh300,000 na mdhamini wa kiasi sawa na hicho kwa kila mmoja.

Mahakama ilielezwa kuwa usiku wa Februari 13 katika eneo la Gatundia, wilayani Laikipia Magharibi, washtakiwa wakiwa na nia ya kutisha familia ya Bw Jackson Mogusu, walisambaza ndumba yao ambayo ilikuwa majani makavu na mifupa iliyovunjika katika boma hilo, huku wakitamka maneno ambayo hayakueleweka kwa nia ya kuroga familia hiyo.

Waliua ng'ombe

Mahakama pia ilifahamishwa kuwa tarehe hiyo, washukiwa waliua ng’ombe na ndama wake masaa ya alfajiri na pia kuingia katika boma la Bw Mogusu bila idhini.

Bi Watila aliambia mahakama kuwa  alikuwa ameajiriwa na mwanamume ambaye sasa ametoweka. Hata hivyo, alikiri kuwa na ndumba hiyo ingawaje alikanusha kuwa zilitumiwa kumroga mlalamishi.

Mahakama iliagiza kesi hiyo isikizwe Machi 16 na kwamba mshtakiwa apelekwe jela la wanawake la Nyahururu baada ya kushindwa kulipa dhamana.

Share Bookmark Print

Rating

 

 

 

 

 

 

Most Popular

Wabunge 175 kutahiriwa Zimbabwe

Wabunge 175 nchini Zimbabwe watapashwa tohara kufikia mwisho wa mwezi ujao katika juhudi za kuhamasisha wanaume

Mwanawe Waziri wa Fedha ajitia kitanzi

MWANAWE Waziri wa Fedha Njeru Githae anadaiwa kujiua nyumbani kwao Runda, Nairobi. Polisi wameanzisha uchunguzi

Polisi waendelea kusaka walioshambulia Mombasa

Polisi wameanzisha msako mkali kutafuta washukiwa waliotekeleza shambulio la kigaidi katika mkahawa wa Bella Vista,

Utengano wakumba ukumbusho wa Wanjiru

Ibada mbili tofauti zilifanywa kuadhimisha mwaka mmoja tangu kifo cha bingwa wa marathon katika Olimpiki Samuel