Aliyechapwa na mkewe aondoa kesi

Mwenyekiti wa chama cha Maendeleo ya Wanaume, Bw Nderitu Njoka.

Picha/MAKTABA Mwenyekiti wa chama cha Maendeleo ya Wanaume, Bw Nderitu Njoka ambaye amekuwa akitetea wanaume akihutubia wanahabari Desemba 17, 2009. 

Na CHARLES MWANIKI  ( email Mwandishi)

Imepakiwa - Wednesday, February 22  2012  at 19:24

Kwa Mukhtasari

Bw Patrick Kimaru Mwangi, aliambia Hakimu Mkuu Mkazi wa Nyeri,  Bi Joan Wambilyanga kwamba alimsamehe mkewe, Bi Eunice Wairema Gaitho, baada ya kuombwa msamaha na kuhakikishiwa kwamba asingechapwa tena.

 

MWANAUME ambaye alikuwa wa kwanza kujitokeza hadharani  kwa kudai kuchapwa na mke wake sasa ametupilia mbali kesi dhidi ya mwanamke huyo mahakamani.

Bw Patrick Kimaru Mwangi, aliambia Hakimu Mkuu Mkazi wa Nyeri,  Bi Joan Wambilyanga kwamba alimsamehe mkewe, Bi Eunice Wairema Gaitho, baada ya kuombwa msamaha na kuhakikishiwa kwamba asingechapwa tena.

Bi Wairema alishtakiwa  Januari 23 kwa madai ya kupiga na kumuumiza Bw Kimaru mnamo Januari 1, katika kijiji cha Ngangarithi, Nyeri.

Wakati Kiongozi wa Mashtaka, Inspekta Bernard Wamalwa alisema kwamba alikwa tayari kuendeleza kesi,  Bi Wairema aliomba kuzungumza, na kueleza kwamba mumewe, ambaye ni msanii mjini Nyeri, alikuwa tayari kuondoa mashtaka hayo dhidi yake.

Hakushurutishwa

Alipoitwa mbele ya korti kuthibitisha ukweli huo, Bw Kimaru alisema kwamba hakushurutishwa na yeyote kuondoa kesi hiyo, bali alifanya hivyo kwa hiari yake.

“Mke wangu ameniomba msamaha na kuniambia kwamba hatarudia kosa hili.  Nimekubali kwani yeye ni mke wangu na sijashurutishwa na yeyote kuondoa mashtaka haya,” akasema Bw Kimaru.

Kwenye kesi nyingine, watu watatu waliioshtakiwa kwa madai ya wizi wa mali kwenye vyumba vya hoteli ya kifahari ya Outspan, wataendelea kuzuiliwa kwenye Kituo cha polisi cha Nyeri hadi Ijumaa kufuatia ombi kutoka kwa upande wa mashtaka.

Share Bookmark Print

Rating

 

 

 

 

 

 

Most Popular

Wabunge 175 kutahiriwa Zimbabwe

Wabunge 175 nchini Zimbabwe watapashwa tohara kufikia mwisho wa mwezi ujao katika juhudi za kuhamasisha wanaume

Mwanawe Waziri wa Fedha ajitia kitanzi

MWANAWE Waziri wa Fedha Njeru Githae anadaiwa kujiua nyumbani kwao Runda, Nairobi. Polisi wameanzisha uchunguzi

Polisi waendelea kusaka walioshambulia Mombasa

Polisi wameanzisha msako mkali kutafuta washukiwa waliotekeleza shambulio la kigaidi katika mkahawa wa Bella Vista,

Utengano wakumba ukumbusho wa Wanjiru

Ibada mbili tofauti zilifanywa kuadhimisha mwaka mmoja tangu kifo cha bingwa wa marathon katika Olimpiki Samuel