UCHUMI NA BIASHARA
Na JOHN SHILITSA ( email Mwandishi)
Imepakiwa - Tuesday, February 14 2012 at 19:35Kwa Mukhtasari
Wachangiaji wasema adhabu ya Sh800 ni juu sana na wakataka Waziri wa Huduma za Matibabu, Prof Anyang Nyong’o kuingilia kati.
SERIKALI imeshauriwa kuondoa adhabu inayotozwa kwa wanaochangia kwa Hazina ya Bima ya Kitaifa ya Matibabu (NHIF), wanapochelewa kulipa.
Wachangiaji ambao hawajaariwa walisema adhabu ya Sh800 ni juu sana na wakataka Waziri wa Huduma za Matibabu, Prof Anyang Nyong’o kuingilia kati.
“Wengi wetu huenda tukakosa kuwa katika bima hiyo ya matibabu,” alisema Bi Angela Mukongolo, ambaye ni mke wa nyumbani.
Uchunguzi wa Taifa Leo katika afisi za NHIF Mumias, ulionyesha kuwa idadi kubwa ya wanaokosa kulipa kwa wakati ni watu ambao hawajaajiriwa. Wengi wao ni wahudumu wa bodaboda na wakulima wakujikimu.
Bi Mukongolo alisema adhabu hiyo inastahili kuangaliwa upya kwa sababu madhumuni ya bima hiyo, hayatafaulu ikiwa wanaolengwa wanawekewa masharti wasiyoweza kutimiza. Wanaokosa kulipa hutozwa kiasi hicho cha pesa kila mwezi kando na mchango wao wa Sh160 kwa mwezi.
Walioathiriwa walidai kuwa wanadaiwa na NHIF kati ya Sh3,500 na Sh7,000 kwa sababu ya kutozwa adhabu hiyo.
Wabunge 175 nchini Zimbabwe watapashwa tohara kufikia mwisho wa mwezi ujao katika juhudi za kuhamasisha wanaume
MWANAWE Waziri wa Fedha Njeru Githae anadaiwa kujiua nyumbani kwao Runda, Nairobi. Polisi wameanzisha uchunguzi
Polisi wameanzisha msako mkali kutafuta washukiwa waliotekeleza shambulio la kigaidi katika mkahawa wa Bella Vista,
Ibada mbili tofauti zilifanywa kuadhimisha mwaka mmoja tangu kifo cha bingwa wa marathon katika Olimpiki Samuel