UCHUMI NA BIASHARA

Baraza la Tana lapinga mpango wa Mumias Sugar

Na MATHIAS RINGA  ( email Mwandishi)

Imepakiwa - Tuesday, February 14  2012  at 19:39

Kwa Mukhtasari

Mwenyekiti wa Baraza la Tana River asema endapo Mumias Sugar itaanzisha ukuzaji miwa katika chemchemi hiyo, huenda wakulima zaidi 50,000 wa mifugo wakaathirika kutokana na kukosa maeneo ya kulisha mifugo.

BARAZA la Tana River limepinga vikali mpango wa Kampuni ya Sukari ya Mumias (MSC), kuanzisha mradi wa uzalishaji miwa katika maeneo ya chemchemi ya mto Tana.

Mwenyekiti wa baraza hilo Salim Golo Gure aliomba kampuni hiyo ifutulie mbali mradi wa kulima miwa katika chemchemi ya mto Tana.

Bw Gure alisema endapo MSC itaanzisha ukuzaji miwa katika chemchemi hiyo, huenda wakulima zaidi 50,000 wa mifugo wakaathirika kutokana na kukosa maeneo ya kulisha mifugo.

Mbali na wafugaji kutoka wilaya za Tana River na Tana Delta, alisema, wafugaji kutoka Mkoa wa Kaskazini Mashariki pia hulisha mifugo yao katika chemchemi hiyo.

Eneo la chemchemi

“Eneo la chemchemi ya Tana, lina umuhimu mkubwa kwa wakazi wa Tana Delta na Tana River kwani mifugo yote hupata malisho na vile vile maji,” alisema.

“Baraza la Tana River linaomba kampuni ya MSC ifutilie mbali mpango wa ulimaji miwa katika maeneo haya ya mto Tana mara moja,” akasema.

“Wakazi wapatao 50,000 ambao ni wafugaji watapoteza riziki zao za kila siku ikiwa mpango huo utatimizwa,” akaonya.

Bw Gure aidha,  alionya kwamba fujo huenda zikazuka iwapo kampuni shughuli hiyo ya ukuzaji.  Wafugaji wa Tana River, Bw Basa Ware, pia alipinga mradi huo wa miwa akisema kwamba itatatiza wafugaji.

Bw Ware alidokeza kuwa wakati wa ukame, ni eneo hilo pekee ambalo hutumika kwa ulishaji wa mifugo kutoka Tana River na Mkoa wa Kaskazini Mashariki.

“Nyakati za ukame mifugo kutoka maeneo ya Tana na hata kutoka maeneo ya Mkoa wa Kaskazini Mashariki hulisha katika eneo hilo,” akaarifu.

Hivi majuzi, Mkurugenzi Mkuu wa MSC, Bw Kidero aliarifu kuwa kampuni hiyo pamoja na Halmashauri ya Maendeleo ya Mito Tana na Athi (TARDA) itakuza miwa katikahektari 16,000 kwenye sehemu hiyo.katika maeneo ya chemchemi ya Tana.

 

Most Popular

Wabunge 175 kutahiriwa Zimbabwe

Wabunge 175 nchini Zimbabwe watapashwa tohara kufikia mwisho wa mwezi ujao katika juhudi za kuhamasisha wanaume

Mwanawe Waziri wa Fedha ajitia kitanzi

MWANAWE Waziri wa Fedha Njeru Githae anadaiwa kujiua nyumbani kwao Runda, Nairobi. Polisi wameanzisha uchunguzi

Polisi waendelea kusaka walioshambulia Mombasa

Polisi wameanzisha msako mkali kutafuta washukiwa waliotekeleza shambulio la kigaidi katika mkahawa wa Bella Vista,

Utengano wakumba ukumbusho wa Wanjiru

Ibada mbili tofauti zilifanywa kuadhimisha mwaka mmoja tangu kifo cha bingwa wa marathon katika Olimpiki Samuel