Na DANIEL MULE ( email Mwandishi)
Imepakiwa - Tuesday, February 21 2012 at 20:50Kwa Mukhtasari
Total Kenya imezindua rasmi taa zinazotumia nishati kutoka kwa jua ili kuchangia katika juhudi za kusaidia uhifadhi wa mazingira.
KAMPUNI ya kuuza mafuta ya Total imezindua rasmi taa zinazotumia nishati kutoka kwa jua ili kuchangia katika kutunza mazingira.
Akizungumza katika warsha ya uzinduzi huo Jumanne, Mkurugenzi Mkuu wa Total nchini, Bw Alexis Vovk, alisema hiyo ni mojawapo ya hatua za kampuni hiyo kutunza mazingira.
“Total imekuwa ikijihusisha na upanzi wa miti na kutoa mafunzo kuhusu usalama barabarani kwa muda. Sasa tumeamua kuuza taa zinazotumia nishati kutoka kwa jua ili kupunguza idadi ya watu wanaotegemea mafuta kuwashia taa au kuendesha jenereta,” alisema Bw Vovk.
Alisema kuwa taa hizo kwa jina 'Total Sola’ zimekuwa zikifanyiwa majaribio tangu 2010 na sasa imebainika kuwa kiwango chake ni cha hali ya juu.
Bw Vovk aliongeza kuwa watu wa viwango vyote vilizingatiwa katika shughuli ya uundaji wa taa hizo.
“Kuna taa za kuanzia Sh999 hadi Sh28,000. Kila taa ni tofauti na ina manufaa yake tofauti na nyingine. Mtu anaweza kununua taa yoyote kulingana na mapato na mahitaji yake,” alisema Bw Vovk.
Masaa manane
Alisema taa aina ya S10 inayouzwa kwa Sh999 inaweza kutoa mwangaza kwa muda wa saa nane baada ya kuwekwa kwenye jua kwa saa sita pekee.
“Taa inayotarajiwa kufanya vyema zaidi ni ile ya S250 inayouzwa kwa Sh3,400. Taa hiyo inatoa mwangaza mara kumi zaidi ya taa za kawaida na inaweza kutumika kuongeza nishati kwenye betri za simu,” alisema Bw Vovk.
Naibu Rais wa Total ulimwenguni katika kitengo cha kutunza mazingira, Bi Manoelle Lepoube, alisema kuwa kuna haja kubwa ya kutafuta njia badala za kuzalisha nishati.
“Ili kujitayarisha kwa siku za usoni, ni muhimu kupanua mawazo yetu kulenga mbinu nyingine zitakazotuwezesha kukimu mahitaji huku tukijua hatuvipunji vizazi vijavyo,” alisema Bi Lepoube.
Wabunge 175 nchini Zimbabwe watapashwa tohara kufikia mwisho wa mwezi ujao katika juhudi za kuhamasisha wanaume
MWANAWE Waziri wa Fedha Njeru Githae anadaiwa kujiua nyumbani kwao Runda, Nairobi. Polisi wameanzisha uchunguzi
Polisi wameanzisha msako mkali kutafuta washukiwa waliotekeleza shambulio la kigaidi katika mkahawa wa Bella Vista,
Ibada mbili tofauti zilifanywa kuadhimisha mwaka mmoja tangu kifo cha bingwa wa marathon katika Olimpiki Samuel